14. Naye BWANA ataonekana juu yao,Na mshale wake utatoka kama umeme;Na Bwana MUNGU ataipiga tarumbeta,Naye atakwenda kwa pepo za kisulisuli za kusini.
15. BWANA wa majeshi atawalinda;Nao watakula na kuyakanyaga mawe ya teo;Nao watakunywa na kufanya kelele kama kwa divai;Nao watajazwa kama mabakuli, kama pembe za madhabahu.
16. Na BWANA, Mungu wao, atawaokoa siku hiyo,Kama kundi la watu wake;Kwa maana watakuwa kama vito vya taji,Vikimeta-meta juu ya nchi yake.