Zab. 9:1-9 Swahili Union Version (SUV)

1. Nitamshukuru BWANA kwa moyo wangu wote;Nitayasimulia matendo yako yote ya ajabu;

2. Nitafurahi na kukushangilia Wewe;Nitaliimbia jina lako, Wewe Uliye juu.

3. Kwa sababu adui zangu hurudi nyuma;Hujikwaa na kuangamia mbele zako.

4. Kwa maana umenifanyia hukumu na hakiUmeketi kitini pa enzi ukihukumu kwa haki.

5. Umewakemea mataifa;Na kumwangamiza mdhalimu;Umelifuta jina lao milele na milele;

6. Adui wamekoma na kuachwa ukiwa milele.Nayo miji yao uliing’oa;Hata kumbukumbu lao limepotea.

7. Bali BWANA atakaa milele,Ameweka kiti chake tayari kwa hukumu.

8. Naye atauhukumu ulimwengu kwa haki;Atawaamua watu kwa adili.

9. BWANA atakuwa ngome kwake aliyeonewa,Naam, ngome kwa nyakati za shida.

Zab. 9