42. Umeutukuza mkono wa kuume wa watesi wake;Umewafurahisha wote wanaomchukia.
43. Pia umeurudisha nyuma ukali wa upanga wake;Wala hukumsimamisha vitani.
44. Umeikomesha fahari yake;Kiti chake cha enzi umekitupa chini.
45. Umezipunguza siku za ujana wake;Umemvika aibu.
46. Ee BWANA, hata lini? Utajificha hata milele?Ghadhabu yako itawaka kama moto?