Zab. 86:3-6 Swahili Union Version (SUV)

3. Wewe, Bwana, unifadhili,Maana nakulilia Wewe mchana kutwa.

4. Uifurahishe nafsi ya mtumishi wako,Maana nafsi yangu nakuinulia Wewe, Bwana.

5. Kwa maana Wewe, Bwana, U mwema,Umekuwa tayari kusamehe,Na mwingi wa fadhili,Kwa watu wote wakuitao.

6. Ee BWANA, uyasikie maombi yangu;Uisikilize sauti ya dua zangu.

Zab. 86