3. Wewe, Bwana, unifadhili,Maana nakulilia Wewe mchana kutwa.
4. Uifurahishe nafsi ya mtumishi wako,Maana nafsi yangu nakuinulia Wewe, Bwana.
5. Kwa maana Wewe, Bwana, U mwema,Umekuwa tayari kusamehe,Na mwingi wa fadhili,Kwa watu wote wakuitao.
6. Ee BWANA, uyasikie maombi yangu;Uisikilize sauti ya dua zangu.