Zab. 82:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Mungu asimama katika kusanyiko la Mungu;Katikati ya miungu anahukumu.

2. Hata lini mtahukumu kwa dhuluma,Na kuzikubali nyuso za wabaya?

3. Mfanyieni hukumu maskini na yatima;Mtendeeni haki aliyeonewa na fukara;

4. Mwokoeni maskini na mhitaji;Mwopoeni mikononi mwa wadhalimu.

5. Hawajui wala hawafahamu, hutembea gizani;Misingi yote ya nchi imetikisika.

Zab. 82