56. Lakini walimjaribu Mungu Aliye juu, wakamwasi,Wala hawakuzishika shuhuda zake.
57. Bali walirudi nyuma, wakahaini kama baba zao;Wakaepea kama upinde usiofaa.
58. Wakamkasirisha kwa mahali pao pa juu,Wakamtia wivu kwa sanamu zao.
59. Mungu akasikia, akaghadhibika,Akamkataa Israeli kabisa.
60. Akaiacha maskani ya Shilo,Hema aliyoiweka katikati ya wanadamu;