Zab. 78:56-60 Swahili Union Version (SUV)

56. Lakini walimjaribu Mungu Aliye juu, wakamwasi,Wala hawakuzishika shuhuda zake.

57. Bali walirudi nyuma, wakahaini kama baba zao;Wakaepea kama upinde usiofaa.

58. Wakamkasirisha kwa mahali pao pa juu,Wakamtia wivu kwa sanamu zao.

59. Mungu akasikia, akaghadhibika,Akamkataa Israeli kabisa.

60. Akaiacha maskani ya Shilo,Hema aliyoiweka katikati ya wanadamu;

Zab. 78