Zab. 78:19-28 Swahili Union Version (SUV)

19. Naam, walimwamba Mungu, wakasema,Je! Mungu aweza kuandika meza jangwani?

20. Tazama, aliupiga mwamba;Maji yakabubujika, ikafurika mito.Pia aweza kutupa chakula?Atawaandalia watu wake nyama?

21. Hivyo BWANA aliposikia akaghadhibika;Moto ukawashwa juu ya Yakobo,Hasira nayo ikapanda juu ya Israeli.

22. Kwa kuwa hawakumwamini Mungu,Wala hawakuutumainia wokovu wake.

23. Lakini aliyaamuru mawingu juu;Akaifungua milango ya mbinguni;

24. Akawanyeshea mana ili wale;Akawapa nafaka ya mbinguni.

25. Mwanadamu akala chakula cha mashujaa;Aliwapelekea chakula cha kuwashibisha.

26. Aliuelekeza upepo wa mashariki mbinguni;Akaiongoza kusi kwa uweza wake.

27. Akawanyeshea nyama kama mavumbi,Na ndege wenye mbawa,Kama mchanga wa bahari.

28. Akawaangusha kati ya matuo yao,Pande zote za maskani zao.

Zab. 78