Zab. 78:10-17 Swahili Union Version (SUV)

10. Hawakulishika agano la Mungu;Wakakataa kuenenda katika sheria yake;

11. Wakayasahau matendo yake,Na mambo yake ya ajabu aliyowaonyesha.

12. Mbele ya baba zao alifanya mambo ya ajabu,Katika nchi ya Misri, konde la Soani.

13. Aliipasua bahari akawavusha;Aliyasimamisha maji mfano wa chungu.

14. Akawaongoza kwa wingu mchana,Na usiku kucha kwa nuru ya moto.

15. Akapasua miamba jangwani;Akawanywesha maji mengi kama maji ya vilindi.

16. Akatokeza na vijito gengeni,Akatelemsha maji kama mito.

17. Lakini wakazidi kumtenda dhambi,Walipomwasi Aliye juu katika nchi ya kiu.

Zab. 78