4. Wanaonichukia bure ni wengiKuliko nywele za kichwa changu.Watakao kunikatilia mbali wamekuwa hodari,Adui zangu kwa sababu isiyo kweli.Hata mimi nalilipishwa kwa nguvuVitu nisivyovichukua.
5. Ee Mungu, unajua upumbavu wangu,Wala hukufichwa dhambi yangu.
6. Wanaokungoja Wewe wasiaibishwe,Kwa ajili yangu, Bwana, MUNGU wa majeshi.Wanaokutafuta Wewe wasifedheheshwe,Kwa ajili yangu, Ee Mungu wa Israeli.