Zab. 31:20-23 Swahili Union Version (SUV)

20. Utawasitiri na fitina za watuKatika sitara ya kuwapo kwako;Utawaficha katika hemaNa mashindano ya ndimi.

21. BWANA ahimidiwe; kwa maana amenitendeaFadhili za ajabu katika mji wenye boma.

22. Nami nalisema kwa haraka yangu,Nimekatiliwa mbali na macho yako;Lakini ulisikia sauti ya dua yanguWakati nilipokulilia.

23. Mpendeni BWANA,Ninyi nyote mlio watauwa wake.BWANA huwahifadhi waaminifu,Humlipa atendaye kiburi malipo tele.

Zab. 31