Zab. 150:2-6 Swahili Union Version (SUV)

2. Msifuni kwa matendo yake makuu;Msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.

3. Msifuni kwa mvumo wa baragumu;Msifuni kwa kinanda na kinubi;

4. Msifuni kwa matari na kucheza;Msifuni kwa zeze na filimbi;

5. Msifuni kwa matoazi yaliayo;Msifuni kwa matoazi yavumayo sana.

6. Kila mwenye pumzi na amsifu BWANA.Haleluya.

Zab. 150