161. Wakuu wameniudhi bure,Ila moyo wangu unayahofia maneno yako.
162. Naifurahia ahadi yako,Kama apataye mateka mengi.
163. Nimeuchukia uongo, umenikirihi,Sheria yako nimeipenda.
164. Mara saba kila siku nakusifu,Kwa sababu ya hukumu za haki yako.
165. Wana amani nyingi waipendao sheria yako,Wala hawana la kuwakwaza.