123. Macho yangu yamefifia kwa kuutamani wokovu wako,Na ahadi ya haki yako.
124. Kama zilivyo rehema zako umtendee mtumishi wako,Na amri zako unifundishe.
125. Mimi ni mtumishi wako, unifahamishe,Nipate kuzijua shuhuda zako.
126. Wakati umewadia BWANA atende kazi;Kwa kuwa wameitangua sheria yako.
127. Ndiyo maana nimeyapenda maagizo yako,Kuliko dhahabu, naam, dhahabu iliyo safi.
128. Maana nayaona mausia yako yote kuwa ya adili,Kila njia ya uongo naichukia.