3. Kamba za mauti zilinizunguka,Shida za kuzimu zilinipata.Naliona taabu na huzuni;
4. Nikaliitia jina la BWANA.Ee BWANA, nakuomba sana,Uniokoe nafsi yangu.
5. BWANA ni mwenye neema na haki,Naam, Mungu wetu ni mwenye rehema.
6. BWANA huwalinda wasio na hila;Nalidhilika, akaniokoa.
7. Ee nafsi yangu, urudi rahani mwako,Kwa kuwa BWANA amekutendea ukarimu.
8. Maana umeniponya nafsi yangu na mauti,Macho yangu na machozi,Na miguu yangu na kuanguka.