1. Ee Mungu wa sifa zangu, usinyamaze,
2. Kwa maana wamenifumbulia kinywa;Kinywa cha mtu asiye haki, cha hila,Wamesema nami kwa ulimi wa uongo.
3. Naam, kwa maneno ya chuki wamenizunguka,Wamepigana nami bure.
4. Badala ya upendo wangu wao hunishitaki,Ijapokuwa naliwaombea.