Zab. 105:20-24 Swahili Union Version (SUV)

20. Mfalme alituma watu akamfungua,Mkuu wa watu akamwachia.

21. Akamweka kuwa bwana wa nyumba yake,Na mwenye amri juu ya mali zake zote.

22. Awafunge masheki wake kama apendavyo,Na kuwafundisha wazee wake hekima.

23. Israeli naye akaingia Misri,Yakobo akawa mgeni katika nchi ya Hamu.

24. Akawajalia watu wake wazae sana,Akawafanya kuwa hodari kuliko watesi wao.

Zab. 105