19. Aliufanya mwezi kwa ajili ya nyakati,Jua latambua kuchwa kwake.
20. Wewe hufanya giza, kukawa usiku,Ndipo atambaapo kila mnyama wa mwitu.
21. Wana-simba hunguruma wakitaka mawindo,Ili kutafuta chakula chao kwa Mungu.
22. Jua lachomoza, wanakwenda zao,Na kujilaza mapangoni mwao.
23. Mwanadamu atoka kwenda zake kazini,Na kwenye utumishi wake mpaka jioni.