Zab. 1:2-5 Swahili Union Version (SUV)

2. Bali sheria ya BWANA ndiyo impendezayo,Na sheria yake huitafakari mchana na usiku.

3. Naye atakuwa kama mti uliopandwaKandokando ya vijito vya maji,Uzaao matunda yake kwa majira yake,Wala jani lake halinyauki;Na kila alitendalo litafanikiwa.

4. Sivyo walivyo wasio haki;Hao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.

5. Kwa hiyo wasio haki hawatasimama hukumuni,Wala wakosaji katika kusanyiko la wenye haki.

Zab. 1