Yn. 8:33-36 Swahili Union Version (SUV)

33. Wakamjibu, Sisi tu uzao wake Ibrahimu, wala hatujawa watumwa wa mtu wakati wo wote; nawe wasemaje, Mtawekwa huru?

34. Yesu akawajibu, Amin, amin, nawaambia, Kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi.

35. Wala mtumwa hakai nyumbani sikuzote; mwana hukaa sikuzote.

36. Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli.

Yn. 8