Yn. 8:13-17 Swahili Union Version (SUV)

13. Basi Mafarisayo wakamwambia, Wewe unajishuhudia mwenyewe; ushuhuda wako si kweli.

14. Yesu akajibu, akawaambia, Mimi ningawa ninajishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu ndio kweli; kwa sababu najua nilikotoka na niendako; lakini ninyi hamjui nilikotoka wala niendako.

15. Ninyi mwahukumu kwa kufuata mambo ya mwili; mimi simhukumu mtu.

16. Nami nijapohukumu, hukumu yangu ni kweli; kwa kuwa mimi si peke yangu, bali ni mimi na yeye aliyenipeleka.

17. Tena katika torati yenu imeandikwa kwamba, Ushuhuda wa watu wawili ni kweli.

Yn. 8