5. Tomaso akamwambia, Bwana, sisi hatujui uendako; nasi twaijuaje njia?
6. Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.
7. Kama mngalinijua mimi, mngalimjua na Baba; tangu sasa mnamjua, tena mmemwona.
8. Filipo akamwambia, Bwana, utuonyeshe Baba, yatutosha.