Yn. 12:10-15 Swahili Union Version (SUV)

10. Nao wakuu wa makuhani wakafanya shauri la kumwua Lazaro naye;

11. maana kwa ajili yake wengi katika Wayahudi walijitenga, wakamwamini Yesu.

12. Nayo siku ya pili yake watu wengi walioijia sikukuu walisikia ya kwamba Yesu anakuja Yerusalemu;

13. wakatwaa matawi ya mitende, wakatoka nje kwenda kumlaki, wakapiga makelele, Hosana! Ndiye mbarikiwa ajaye kwa jina la Bwana, Mfalme wa Israeli!

14. Naye Yesu alikuwa amepata mwana-punda, akampanda, kama vile iliyoandikwa,

15. Usiogope, binti Sayuni; tazama, Mfalme wako anakuja, amepanda mwana-punda.

Yn. 12