10. Nao wakuu wa makuhani wakafanya shauri la kumwua Lazaro naye;
11. maana kwa ajili yake wengi katika Wayahudi walijitenga, wakamwamini Yesu.
12. Nayo siku ya pili yake watu wengi walioijia sikukuu walisikia ya kwamba Yesu anakuja Yerusalemu;
13. wakatwaa matawi ya mitende, wakatoka nje kwenda kumlaki, wakapiga makelele, Hosana! Ndiye mbarikiwa ajaye kwa jina la Bwana, Mfalme wa Israeli!
14. Naye Yesu alikuwa amepata mwana-punda, akampanda, kama vile iliyoandikwa,
15. Usiogope, binti Sayuni; tazama, Mfalme wako anakuja, amepanda mwana-punda.