Yn. 11:17-21 Swahili Union Version (SUV)

17. Basi Yesu alipofika, alimkuta amekwisha kuwamo kaburini yapata siku nne.

18. Na Bethania ilikuwa karibu na Yerusalemu, kadiri ya maili mbili hivi;

19. na watu wengi katika Wayahudi walikuwa wamekuja kwa Martha na Mariamu, ili kuwafariji kwa habari ya ndugu yao.

20. Basi Martha aliposikia kwamba Yesu anakuja, alikwenda kumlaki; na Mariamu alikuwa akikaa nyumbani.

21. Basi Martha akamwambia Yesu, Bwana, kama ungalikuwapo hapa, ndugu yangu hangalikufa.

Yn. 11