Yer. 51:41-44 Swahili Union Version (SUV)

41. Jinsi Sheshaki alivyotwaliwa!Naye sifa ya dunia yote alivyoshambuliwa!Jinsi Babeli alivyokuwa ukiwaKatikati ya mataifa!

42. Bahari imefika juu ya Babeli,Umefunikwa kwa wingi wa mawimbi yake.

43. Miji yake imekuwa maganjo;Nchi ya ukame, na jangwa;Nchi asimokaa mtu ye yote,Wala hapiti mwanadamu huko.

44. Nami nitafanya hukumu juu ya Beli katika Babeli, nami nitavitoa katika kinywa chake alivyovimeza; wala mataifa hawatamwendea tena; naam, ukuta wa Babeli utaanguka.

Yer. 51