15. Ameiumba dunia kwa uweza wake,Ameuthibitisha ulimwengu kwa hekima yake,Na kwa ufahamu wake amezitandika mbingu.
16. Atoapo sauti yake pana mshindo wa maji mbinguni,Naye hupandisha mawingu toka ncha za nchi;Huifanyia mvua umeme,Huutoa upepo katika hazina zake.
17. Kila mtu amekuwa kama mnyama, hana maarifa;Kila mfua dhahabu amefedheheshwa na sanamu yake ya kuchonga;Maana sanamu yake ya kuyeyuka ni uongo,Wala hamna pumzi ndani yake.
18. Ni ubatili tu, ni kazi za udanganyifu;Wakati wa kujiliwa kwao watapotea.