2. Tangazeni katika mataifa,Mkahubiri na kutweka bendera;Hubirini, msifiche, semeni,Babeli umetwaliwa!Beli amefedheheka;Merodaki amefadhaika;Sanamu zake zimeaibishwa,Vinyago vyake vimefadhaika.
3. Maana toka kaskazini taifa linakuja juu yake, litakaloifanya nchi yake kuwa ukiwa; wala hapana mtu atakayekaa humo; wamekimbia, wamekwenda zao, mwanadamu na mnyama pia.
4. Katika siku hizo, na wakati huo, asema BWANA, wana wa Israeli watakuja, wao na wana wa Yuda pamoja; Wataendelea njiani mwao wakilia, nao watamtafuta BWANA, Mungu wao.