Yer. 50:10-12 Swahili Union Version (SUV)

10. Nao Ukaldayo utakuwa mateka; wote wautekao watashiba, asema BWANA.

11. Kwa sababu mnafurahi, kwa sababu mnashangilia, enyi mnaouteka urithi wangu, kwa sababu mmewanda kama mtamba akanyagaye nafaka, nanyi mnalia kama farasi wenye nguvu;

12. mama yenu atatahayarika sana; yeye aliyewazaa atafadhaika; tazama, atakuwa taifa lililo nyuma katika mataifa yote, atakuwa jangwa, nchi ya ukame, na nyika.

Yer. 50