1. Tena, neno la BWANA likamjia Yeremia mara ya pili, hapo alipokuwa akali amefungwa katika uwanda wa walinzi, kusema,
2. BWANA alitendaye jambo hili, BWANA aliumbaye ili alithibitishe; BWANA ndilo jina lake; asema hivi,
3. Niite, nami nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua.