Yer. 29:28-31 Swahili Union Version (SUV)

28. ambaye ametuma watu kwetu katika Babeli, kusema, Uhamisho huu ni wa siku nyingi; jengeni nyumba, mkakae ndani yake; pandeni bustani, mkale matunda yake.

29. Na Sefania, kuhani, akasoma barua hii masikioni mwa Yeremia nabii.

30. Ndipo neno la BWANA likamjia Yeremia, kusema,

31. Uwapelekee habari watu wote waliohamishwa, kusema, BWANA asema hivi, katika habari za Shemaya, Mnehelami; Kwa sababu Shemaya amewatabiria ninyi, lakini sikumtuma mimi, naye amewatumainisha neno la uongo;

Yer. 29