Yer. 20:13-16 Swahili Union Version (SUV)

13. Mwimbieni BWANA; msifuni BWANA;Kwa maana ameiponya roho ya mhitajiKatika mikono ya watu watendao maovu.

14. Na ilaaniwe siku niliyozaliwa, isibarikiwe siku ile aliyonizaa mama yangu.

15. Na alaaniwe mtu yule aliyemletea baba yangu habari, akisema, Umezaliwa mtoto mwanamume; akimfurahisha.

16. Mtu huyo na awe kama miji ile, ambayo BWANA aliiangamiza, asijute; na asikie kilio asubuhi, na kelele za fujo adhuhuri;

Yer. 20