Wim. 5:2-5 Swahili Union Version (SUV)

2. Nalikuwa nimelala, lakini moyo wangu u macho,Sikiliza! Mpendwa wangu anabisha!Nifungulie, umbu langu, mpenzi wangu,Hua wangu, mkamilifu wangu,Kwa maana kichwa changu kimelowa umande,Nywele zangu zina manyunyu ya usiku.

3. Nimeivua kanzu yangu; niivaeje?Nimeitawadha miguu; niichafueje?

4. Mpendwa wangu aliutia mkono wake tunduni,Na moyo wangu ukachomeka kwa ajili yake.

5. Nikaondoka nimfungulie mpendwa wangu;Mikono yangu ilidondoza manemane,Na vidole vyangu matone ya manemane,Penye vipini vya komeo.

Wim. 5