Ufu. 22:7-9 Swahili Union Version (SUV)

7. Na tazama, naja upesi; heri yeye ayashikaye maneno ya unabii wa kitabu hiki.

8. Nami Yohana ndimi niliyeyasikia na kuyaona mambo hayo. Na hapo nilipoyasikia na kuyaona nalianguka, ili nisujudu mbele ya miguu ya malaika yule mwenye kunionyesha hayo.

9. Naye akaniambia, Angalia, usifanye hivi; mimi ni mjoli wako, na wa ndugu zako manabii, na wa wale wayashikao maneno ya kitabu hiki. Msujudie Mungu.

Ufu. 22