Tit. 2:2-6 Swahili Union Version (SUV)

2. ya kwamba wazee wawe wenye kiasi, wastahivu, wenye busara, wazima katika imani na katika upendo na katika saburi.

3. Vivyo hivyo na wazee wa kike wawe na mwenendo wa utakatifu; wasiwe wasingiziaji, wasiwe wenye kutumia mvinyo nyingi, bali wafundishao mema;

4. ili wawatie wanawake vijana akili, wawapende waume zao, na kuwapenda watoto wao;

5. na kuwa wenye kiasi, kuwa safi, kufanya kazi nyumbani mwao, kuwa wema, kuwatii waume zao wenyewe; ili neno la Mungu lisitukanwe.

6. Vivyo hivyo na vijana waume uwaonye kuwa na kiasi;

Tit. 2