Rum. 3:10-17 Swahili Union Version (SUV)

10. kama ilivyoandikwa, ya kwamba,Hakuna mwenye haki hata mmoja.

11. Hakuna afahamuye;Hakuna amtafutaye Mungu.

12. Wote wamepotoka, wameoza wote pia;Hakuna mtenda mema, la! Hata mmoja.

13. Koo lao ni kaburi wazi,Kwa ndimi zao wametumia hila.Sumu ya fira i chini ya midomo yao.

14. Vinywa vyao vimejaa laana na uchungu.

15. Miguu yao ina mbio kumwaga damu.

16. Uharibifu na mashaka yamo njiani mwao.

17. Wala njia ya amani hawakuijua.

Rum. 3