Rum. 15:16-18 Swahili Union Version (SUV)

16. ili niwe mhudumu wa Kristo Yesu kati ya watu wa Mataifa, niifanyie Injili ya Mungu kazi ya ukuhani, kusudi Mataifa wawe sadaka yenye kibali, ikiisha kutakaswa na Roho Mtakatifu.

17. Basi, nina sababu ya kuona fahari katika Kristo Yesu mbele za Mungu.

18. Maana sitathubutu kutaja neno asilolitenda Kristo kwa kazi yangu, Mataifa wapate kutii, kwa neno au kwa tendo,

Rum. 15