7. Imekuwaje basi? Kitu kile ambacho Israeli alikuwa akikitafuta hakukipata; lakini wale waliochaguliwa walikipata, na wengine walitiwa uzito.
8. Kama ilivyoandikwa, Mungu aliwapa roho ya usingizi, macho hata wasione, na masikio hata wasisikie, hata siku hii ya leo.
9. Na Daudi asema,Meza yao na iwe tanzi na mtego,Na kitu cha kuwakwaza, na malipo kwao;
10. Macho yao yatiwe giza ili wasione,Ukawainamishe mgongo wao siku zote.