11. Huwatia jeuri wanawake katika Sayuni;Na mabikira katika miji ya Yuda.
12. Wakuu hutungikwa kwa mikono yao;Nyuso za wazee hazipewi heshima.
13. Vijana huyachukua mawe ya kusagia;Na watoto hujikwaa chini ya kuni.
14. Wazee wameacha kwenda langoni;Na vijana kwenda ngomani.
15. Furaha ya mioyo yetu imekoma;Machezo yetu yamegeuka maombolezo.
16. Taji ya kichwa chetu imeanguka;Ole wetu! Kwa kuwa tumetenda dhambi.