9. Heri wale waliouawa kwa upangaKuliko wao waliouawa kwa njaa;Maana hao husinyaa, wakichomwaKwa kukosa matunda ya mashamba.
10. Mikono ya wanawake wenye hurumaImewatokosa watoto wao wenyewe;Walikuwa ndio chakula chaoKatika uharibifu wa binti ya watu wangu.
11. BWANA ameitimiza kani yake,Ameimimina hasira yake kali;Naye amewasha moto katika SayuniUlioiteketeza misingi yake.