Omb. 4:13-17 Swahili Union Version (SUV)

13. Ni kwa sababu ya dhambi za manabii wakeNa maovu ya makuhani wake,Walioimwaga damu ya wenye hakiKatikati yake.

14. Hutanga-tanga njiani kama vipofu,Wametiwa unajisi kwa damu;Hata ikawa watu wasiwezeKuyagusa mavazi yao.

15. Watu waliwapigia kelele, Ondokeni, Uchafu,Ondokeni, ondokeni, msiguse;Walipokimbia na kutanga-tanga, watu walisema kati ya mataifa,Hawatakaa hapa tena.

16. Hasira ya BWANA imewatenga,Yeye hatawaangalia tena;Hawakujali nafsi za wale makuhani,Hawakuwaheshimu wazee wao.

17. Macho yetu yamechokaKwa kuutazamia bure msaada wetu;Katika kungoja kwetu tumengojea taifaLisiloweza kutuokoa.

Omb. 4