47. Hofu imetujilia na shimo,Ukiwa na uharibifu.
48. Jicho langu lachuruzika mito ya majiKwa ajili ya uvunjifu wa binti ya watu wangu.
49. Jicho langu latoka machozi lisikome,Wala haliachi;
50. Hata BWANA atakapoangaliaNa kutazama toka mbinguni.
51. Jicho langu lanitia huzuni nafsini mwangu,Kwa sababu ya binti zote za mji wangu.
52. Walio adui zangu bila sababuWameniwinda sana kama ndege;