13. Amenichoma viunoKwa mishale ya podo lake.
14. Nimekuwa dhihaka kwa watu wangu wote;Wimbo wao mchana kutwa.
15. Amenijaza uchungu,Amenikinaisha kwa pakanga.
16. Amenivunja meno kwa changarawe;Amenifunika majivu.
17. Umeniweka nafsi yangu mbali na amani;Nikasahau kufanikiwa.