1. Jinsi mji huu ukaavyo ukiwa,Huo uliokuwa umejaa watu!Jinsi alivyokuwa kama mjane,Yeye aliyekuwa mkuu kati ya mataifa!Binti mfalme kati ya majimbo,Jinsi alivyoshikwa shokoa!
2. Hulia sana wakati wa usiku,Na machozi yake yapo mashavuni;Miongoni mwa wote waliompendaHakuna hata mmoja amfarijiye;Rafiki zake wote wamemtenda hila,Wamekuwa adui zake.
3. Yuda amehamishwa kwa sababu ya kuonewa,Na kwa sababu ya utumwa mkuu;Anakaa kati ya makafiri,Haoni raha iwayo yote;Wote waliomfuata wamempataKatika dhiki yake.
4. Njia za Sayuni zaomboleza,Kwa kuwa hakuna ajaye kwa sikukuu;Malango yake yote yamekuwa ukiwa,Makuhani wake hupiga kite;Wanawali wake wanahuzunika;Na yeye mwenyewe huona uchungu.