16. Yusufu akamjibu Farao, akisema, Si mimi; Mungu atampa Farao majibu ya amani.
17. Farao akamwambia Yusufu, Katika ndoto yangu nalikuwa nikisimama ukingoni mwa mto;
18. na tazama, ng’ombe saba wanatoka mtoni, wanono, wazuri, wakajilisha manyasini.
19. Kisha, tazama, ng’ombe saba wengine wakapanda baada yao, dhaifu, wabaya sana, wamekonda; katika nchi yote ya Misri sijaona kama hao kwa udhaifu.
20. Na hao ng’ombe waliokonda, wabaya, wakawala wale ng’ombe saba wa kwanza, wale wanono.