Mwa. 30:10-14 Swahili Union Version (SUV)

10. Zilpa, mjakazi wa Lea, akamzalia Yakobo mwana.

11. Lea akasema, Bahati njema! Akamwita jina lake Gadi.

12. Zilpa, mjakazi wa Lea, akamzalia Yakobo mwana wa pili.

13. Lea akasema, Ni heri mimi, maana wanawake wataniita heri. Akamwita jina lake Asheri.

14. Reubeni akaenda siku za mavuno ya ngano akaona tunguja kondeni, akazileta kwa Lea mamaye. Ndipo Raheli akamwambia Lea, Nipe mimi baadhi ya tunguja za mwanao.

Mwa. 30