Mwa. 18:20-23 Swahili Union Version (SUV)

20. BWANA akasema, Kwa kuwa kilio cha Sodoma na Gomora kimezidi, na dhambi zao zimeongezeka sana,

21. basi, nitashuka sasa nione kama wanayotenda ni kiasi cha kilio kilichonijia; na kama sivyo, nitajua.

22. Basi wale watu wakatoka huko wakaelekea Sodoma; lakini Ibrahimu alikuwa akali akisimama mbele za BWANA.

23. Ibrahimu akakaribia, akasema, Je! Utaharibu mwenye haki pamoja na mwovu?

Mwa. 18