10. Mwanzo wa ufalme wake ulikuwa Babeli na Ereku, na Akadi, na Kalne, katika nchi ya Shinari.
11. Akatoka katika nchi ile akaenda mpaka Ashuru, akajenga Ninawi, na Rehoboth-iri, na Kala;
12. na Reseni, kati ya Ninawi na Kala, nao ni mji mkubwa.
13. Misri akazaa Waludi, na Waanami, na Walehabi, na Wanaftuhi,
14. na Wapathrusi, na Wakasluhi; huko ndiko walikotoka Wafilisti na Wakaftori.
15. Kanaani akamzaa Sidoni, mwanawe wa kwanza, na Hethi,
16. na Myebusi, na Mwamori, na Mgirgashi,