1. Siku zile aliondokea Yohana Mbatizaji akihubiri katika nyika ya Uyahudi, na kusema,
2. Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia.
3. Kwa sababu huyo ndiye aliyenenwa na nabii Isaya, akisema,Sauti ya mtu aliaye nyikani,Itengenezeni njia ya Bwana,Yanyosheni mapito yake.