Mt. 25:35-40 Swahili Union Version (SUV)

35. kwa maana nalikuwa na njaa, mkanipa chakula; nalikuwa na kiu, mkaninywesha; nalikuwa mgeni, mkanikaribisha;

36. nalikuwa uchi, mkanivika nalikuwa mgonjwa, mkaja kunitazama; nalikuwa kifungoni, mkanijia.

37. Ndipo wenye haki watakapomjibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona una njaa, tukakulisha, au una kiu tukakunywesha?

38. Tena ni lini tulipokuona u mgeni, tukakukaribisha, au u uchi, tukakuvika?

39. Ni lini tena tulipokuona u mgonjwa, au kifungoni, tukakujia?

40. Na Mfalme atajibu, akiwaambia, Amin, nawaambia, kadiri mlivyomtendea mmojawapo wa hao ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi.

Mt. 25