Mt. 23:8-14 Swahili Union Version (SUV)

8. Bali ninyi msiitwe Rabi, maana mwalimu wenu ni mmoja, nanyi nyote ni ndugu.

9. Wala msimwite mtu baba duniani; maana Baba yenu ni mmoja, aliye wa mbinguni.

10. Wala msiitwe viongozi; maana kiongozi wenu ni mmoja, naye ndiye Kristo.

11. Naye aliye mkubwa wenu atakuwa mtumishi wenu.

12. Na ye yote atakayejikweza, atadhiliwa; na ye yote atakayejidhili, atakwezwa.

13. Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnawafungia watu ufalme wa mbinguni; ninyi wenyewe hamwingii, wala wanaoingia hamwaachi waingie.

14. [Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnakula nyumba za wajane, na kwa unafiki mnasali sala ndefu; kwa hiyo mtapata hukumu iliyo kubwa zaidi.]

Mt. 23