Mt. 21:16-19 Swahili Union Version (SUV)

16. wakamwambia, Wasikia hawa wasemavyo? Yesu akawaambia, Naam; hamkupata kusoma, Kwa vinywa vya watoto wachanga na wanyonyao umekamilisha sifa?

17. Akawaacha, akatoka nje ya mji mpaka Bethania, akalala huko.

18. Hata asubuhi alipokuwa akienda mjini, aliona njaa.

19. Akaona mtini mmoja kando ya njia, akauendea, asione kitu juu yake ila majani tu; akauambia, Yasipatikane matunda kwako tangu leo hata milele. Mtini ukanyauka mara.

Mt. 21